Huenda umepatana au kumwona mtu asiye na uwezo wa kuona. Wengi wao hutumia mikono kusoma, wakitumia mfumo wa breli. Hata hivyo, si kila wakati hilo hushuhudiwa. Kutana na mwanafunzi mmoja, kwa jina Irene Nthambi, kutoka shule ya msingi ya wanafunzi walio na ulemavu wa kutoona huko Thika. Ajabu, kando na kuwa katika hali hiyo, yeye hawezi kutumia mikono yake kuandika, baada ya kupatwa na ugonjwa wa sukari. Hata hivyo, amebuni namna ya kusoma, akitumia mdomo wake. Linaloshangaza, ni namna anavyoandika, na kusoma, na utabaki kumtazama kwa mshangao kuhusu ustadi wake usijue la kusema. Huyu hapa Nancy Onyancha, na maelezo zaidi kwenye makala kinywa changu, uhai wangu.
Related Articles

December 13, 2019
2,606
Watu 20 wakimbizwa hospitalini baada ya kudaiwa kula Githeri yenye sumu Baringo
Check Also
Close-
Gavana Sonko aachiliwa kwa dhamana ya Ksh 15m pesa taslimu
December 11, 2019